KIYOA's EVENTS/ MATUKIO MBALIMBALI YA KIYOA
VIDOKEZO VIHUSUVYO DARAJA LA KIGAMBONI
Kuanza kwa Ujenzi
Ujenzi
wake ulizinduliwa rasmi tarehe 20 Septemba, 2012 na Mhe. Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete ambaye ni Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Malengo Makuu ya Ujenzi wa Daraja
Malengo makuu ya
ujenzi huu, ni kusaidia kupunguza msongamano wa magari ambayo hupita
katikati ya jiji la Dar es salaam wakati yakienda au yakitoka eneo la Kigamboni; Lengo lingine ni kurahisisha usafiri wa watu pamoja na mazao kwa wakazi wa kigamboni na pia kuongeza utalii
wa pwani ya kusini mwa mkoa wa DSM yaani eneo la Kigamboni.
Visifa Vikuu ya Daraja
-
Daraja
hilo litakapokamilika litakuwa na urefu
wa mita 680;
-
Litakuwa na njia sita na magari
yatalipia wakati yanavuka bahari yakitumia daraja;
-
Hakuna
malipo kwa watembea kwa miguu na baiskeli;
-
Ujenzi
wake utagharimu Bilioni 214.6 mpaka utakapokamilika; na
-
40% ya fedha inatolewa na Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na 60% inatolewa na Mfuko wa Hifadhi ya Jamii wa NSSF.
Kuisha kwa Ujenzi
- Ujenzi wa daraja hili umepangwa kukamilika
tarehe 1 Februari, 2015.
Pichani juu ni namna daraja la Kigamboni litakavyoonekana.
Pichani juu anayeonekana akifungua jiwe la msingi ni Mhe. Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania siku alipokuwa akizindua ujenzi wa daraja la Kigamboni, tarehe 20 Septemba, 2012.
Ahsante mdau kwa kupenda kujua mabadiliko yanayoendea Kigamboni.
UJUMBE WA LEO
HOJA BINAFSI