KIYOA WAHITIMU MAFUNZO YAHUSUYO MAHUSIANO NA MAWASILIANO KATIKA JAMII (KIVUKO)- TAREHE 30 MEI, 2008.
Pichani chini ni baadhi ya WanaKIYOA wakipokea vyeti vya kuhitimu mafunzo ya mahusiano na mawasiliano (mafunzo yajulikanayo kwa jina la KIVUKO) kutoka kwa Walimu kutoka PASADA. Ilikuwa ni tarehe 30 Mei, 2008.
KIYOA inawashukuru sana PASADA kwa mafunzo haya muhimu yanayoendelea kutuunganisha pamoja vijana na kutuwezesha kuishi vyema zaidi katika jamii katika maisha yetu ya kila siku.
Pichani juu ni dada Donatha Mwita akipokea cheti chake cha kuhitimu mafunzo ya
KIVUKO.
Pichani juu ni dada Ghati F. Changarawe akipokea cheti.
Pichani juu ni kaka Greyson Mwikola akipokea cheti chake. Vilevile, vijana wanaoonekana
pichani hapo chini ni baadhi ya Wanakiyoa wakionyesha vyeti walivyopokea siku hiyo.