KIYOA PROFILE / IFAHAMU KIYOA

P.O. Box 36109, Tungi, Kigamboni, Dar es salaam, Tanzania
KAULI MBIU:- Umoja; Upendo na Maendeleo

Thursday, February 21, 2013



ZOEZI LA USAFI WA MAZINGIRA LILILOFANYIKA TAREHE 16 FEBRUARI, 2013





 

Pichani juu ni baadhi ya vijana wa KIYOA wakianza utekelezaji wa ukusanyaji na uchomaji  takataka   zilizoonekana katika maeneo yanayozunguka nyumba za wakazi wa Tungi Kigamboni, Dar es Salaam. Lengo kuu la zoezi hili lilikuwa ni kuwakumbusha Wananchi juu ya umihimu wa ushiriki wa pamoja katika utunzaji wa mazingira yanayotuzunguka.





Pichani juu ni dada Joanitha Joas akiendelea na ukusanyaji wa takataka zilizosambaa katika makazi ya watu.

 

Pichani chini ni Wadada wa KIYOA wakiendelea na zoezi la ukusanyaji na uchomaji takataka.

 


Pichani  chini, zoezi la ukusanyaji na uchomaji takataka likiendelea katika eneo lililo katikati ya makazi ya watu na ambalo limekuwa likitumika kama dampo la takataka.




   Zoezi la ukusanyaji na uchomaji takataka hatua ya kwanza  lakamilika.  




UJUMBE KWA WANAJAMII


NI VYEMA SOTE KWA PAMOJA TUZINGATIE MAELEKEZO NA KANUNI ZA AFYA BORA KWA KUSHIRIKI  KATIKA UTUNZAJI MAZINGIRA YETU YANAYOTUZUNGUKA.

Aidha, kwa wakazi wa Tungi, Kigamboni Dar es Salaam. KIYOA inapenda kuwajulisha kuwa, utaratibu maalum wa ukusanyaji wa takataka umeandaliwa ambapo KIYOA wakishirikiana na FEDERATION watapita majumbani na kukusanya takataka zote zilizozalishwa kwenda kutupwa eneo lililoteuliwa. Wana-Tungi wote mnaombwa kutoa ushirikiano wakati wa zoezi hili. 

No comments:

Post a Comment