ZOEZI LA USAFI WA MAZINGIRA LILILOFANYIKA TAREHE 16 FEBRUARI, 2013
Pichani juu ni baadhi ya vijana wa KIYOA wakianza utekelezaji wa ukusanyaji na uchomaji takataka zilizoonekana katika maeneo yanayozunguka nyumba za wakazi wa Tungi Kigamboni, Dar es Salaam. Lengo kuu la zoezi hili lilikuwa ni kuwakumbusha Wananchi juu ya umihimu wa ushiriki wa pamoja katika utunzaji wa mazingira yanayotuzunguka.
Pichani juu ni dada Joanitha Joas akiendelea na ukusanyaji wa takataka zilizosambaa katika makazi ya watu.
Pichani chini ni Wadada wa KIYOA wakiendelea na zoezi la ukusanyaji na uchomaji takataka.
Pichani chini, zoezi la ukusanyaji na uchomaji takataka likiendelea katika eneo lililo katikati ya makazi ya watu na ambalo limekuwa likitumika kama dampo la takataka.
Zoezi la ukusanyaji na uchomaji takataka hatua ya kwanza lakamilika.
UJUMBE KWA WANAJAMII
NI VYEMA SOTE KWA PAMOJA TUZINGATIE MAELEKEZO NA KANUNI ZA AFYA BORA KWA KUSHIRIKI KATIKA UTUNZAJI MAZINGIRA YETU YANAYOTUZUNGUKA.
No comments:
Post a Comment