KIYOA PROFILE / IFAHAMU KIYOA

P.O. Box 36109, Tungi, Kigamboni, Dar es salaam, Tanzania
KAULI MBIU:- Umoja; Upendo na Maendeleo

Wednesday, September 4, 2013

Monday, July 29, 2013

Thursday, May 30, 2013

KUMBUKUMBU  (LEO ZAMANI)

KIYOA WAHITIMU MAFUNZO YAHUSUYO MAHUSIANO NA MAWASILIANO KATIKA JAMII (KIVUKO)- TAREHE 30 MEI, 2008.

Pichani chini ni baadhi ya WanaKIYOA wakipokea vyeti vya kuhitimu mafunzo ya mahusiano na mawasiliano (mafunzo yajulikanayo kwa jina la KIVUKO) kutoka kwa Walimu kutoka PASADA. Ilikuwa ni tarehe 30 Mei, 2008. 


KIYOA inawashukuru sana PASADA kwa mafunzo haya muhimu yanayoendelea kutuunganisha pamoja vijana na kutuwezesha kuishi vyema zaidi katika jamii katika maisha yetu ya kila siku.





    Pichani juu ni dada Donatha Mwita akipokea cheti chake cha kuhitimu mafunzo ya    
    KIVUKO.




   Pichani juu ni dada Ghati F. Changarawe akipokea cheti.




    Pichani juu ni kaka Greyson Mwikola akipokea cheti chake. Vilevile, vijana wanaoonekana
    pichani hapo chini ni baadhi ya Wanakiyoa wakionyesha vyeti walivyopokea siku hiyo.

















Tuesday, April 30, 2013

Friday, March 29, 2013


VIDOKEZO  VIHUSUVYO DARAJA LA KIGAMBONI



Kuanza kwa Ujenzi

 

Ujenzi wake ulizinduliwa rasmi tarehe 20 Septemba, 2012 na Mhe. Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete ambaye ni Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.



Malengo Makuu ya Ujenzi wa Daraja

 

Malengo makuu ya ujenzi huu, ni kusaidia kupunguza msongamano         wa magari ambayo hupita katikati ya jiji la Dar es salaam wakati yakienda au yakitoka eneo la Kigamboni; Lengo lingine ni  kurahisisha usafiri wa watu pamoja na   mazao kwa wakazi wa kigamboni  na  pia kuongeza utalii wa pwani ya kusini mwa mkoa wa   DSM yaani eneo la Kigamboni.



Visifa Vikuu ya Daraja

-          Daraja hilo litakapokamilika litakuwa na  urefu wa mita 680;

-          Litakuwa na njia sita na magari yatalipia wakati yanavuka bahari yakitumia daraja;

-          Hakuna malipo kwa watembea kwa miguu na baiskeli;

-          Ujenzi wake utagharimu Bilioni 214.6 mpaka utakapokamilika; na

-          40% ya fedha inatolewa na Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na 60% inatolewa na     Mfuko wa Hifadhi ya Jamii wa NSSF.



Kuisha kwa Ujenzi

-    Ujenzi wa daraja hili umepangwa kukamilika tarehe 1 Februari, 2015.



    Pichani juu ni namna daraja la Kigamboni litakavyoonekana.






Pichani juu anayeonekana akifungua jiwe la msingi ni Mhe. Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania siku alipokuwa akizindua ujenzi wa daraja la Kigamboni, tarehe 20 Septemba, 2012. 

 

Chanzo cha habari – www.tanroards.org

 

Ahsante mdau kwa kupenda kujua mabadiliko yanayoendea Kigamboni.

Thursday, February 28, 2013

 KIJANA CHACHU YA MAENDELEO 


Maendeleo ni moja ya kiashiria muhimu wakati wa utekelezaji wa Dira na Dhamira ya KIYOA. Kwa mujibu wa KIYOA,  "Maendeleo" ni  "hali ya mtu au kundi la watu kufanikiwa kiuchumi na kijamii". Aidha, kufanikiwa kiuchumi inahusisha hali ya kujiongezea kipato kwa njia za halali wakati kufanikiwa kijamii inahusisha kuishi maisha shirikishi ambayo jamii inaweza kutatua changamoto inazozikabili kwa kupitia ushiriki wa watu wake wakati wa kutatua changamoto husika.

 

Kimsingi, kuna changamoto nyingi zinazowakabili watu katika jamii zao, vile vile changamoto hizi hutofautiana kutoka jamii moja hadi nyingine. Mfano, jamii moja wakati inakabiliwa na ujinga, elimu duni, maradhi, n.k, wakati huo huo jamii  nyingine inakabiliwa na majanga kama vile vita vya wenyewe kwa wenyewe, mafuriko ya maji, vimbunga, matetemeko ya ardhi, n.k.

 

Katika baadhi ya maeneo hapa nchini, jamii zetu zimekuwa zikikabiliwa na changamoto mbalimbali ambazo zimekuwa ni vikwazo vya maendeleo katika maeneo husika. Baadhi ya changamoto hizi ni pamoja na utumiaji wa madawa na kulevya, maradhi mbalimbali, uharibifu wa mazingira, uwezo mdogo wa kujikimu kimaisha, ufinyu wa bajeti katika kutekeleza mipango ya maendeleo, n.k.

 

Pamoja na jitihada  zinazochukuliwa na Serikali ikiwemo kutoa elimu katika kupambana na changamoto husika, mwamko mdogo kwa baadhi ya Wanajamii hususan vijana (nguvukazi ya taifa la leo) katika kujitoa kushiriki kikamilifu kusaidiana na jamii ni moja ya changamoto kubwa ndani ya jamii  zilizo nyingi, changamoto hii imekuwa  ni kikwazo kikubwa kwa jamii husika katika kujiletea maendeleo endelevu kupitia njia ya kujitolea. 

 

Ili tuweze kutimiza azma ya "Maendeleo Endelevu" kwa taifa letu, ni vyema vijana sasa popote tulipo tujiunge pamoja katika vikundi vya kijamii na kutumia ujuzi, taaluma na sehemu ya muda  tulionao katika kisaidia juhudi za maendeleo katika jamii zetu tunazoishi. 

 

Vijana ni vyema tukafahamu kuwa,  sote kwa pamoja tuna jukumu kubwa katika kujenga jamii bora kwa kutumia sehemu ya muda wetu, ubunifu, ujuzi , taaluma na elimu tulizonazo  kwa kuwa "Vijana ni Chachu ya Maendeleo katika  Jamii Tunazioshi."

 
 VIJANA TUKIAMUA!! TUNAWEZA!!
   
  

Pichani juu na chini ni baadhi ya vijana wa KIYOA wakiwashirikisha kupanda miti  wanafunzi wa Shule ya Sekondari ya Kata ya Tungi. Zoezi hilo la upandaji miti liligharimiwa na kusimamiwa na KIYOA ikiwa ni sehemu ya uboreshaji mazingira yanayoizunguka shule hiyo.

 
 
 
 

Pichani chini zoezi hilo likiendelea, wanaoonekana ni baadhi ya vijana wa KIYOA wakiwashirikisha kupanda miti walimu wa Shule ya Sekondari ya Kata ya Tungi.

 


 

Monday, February 25, 2013

KIYOA NA FEDERATION KATIKA USAFI WA MAZINGIRA TAREHE  --- 23 FEBRUARI, 2013

 

WanaKIYOA wakishirikiana na kikundi cha FEDERATION (Kikundi cha kijamii chenye makazi yake Tungi, Kigamboni), wameendelea na zoezi la usafi wa mazinngira katika eneo lililopo jirani na Shule ya Msingi Tungi, Kigamboni Dar es salaam. Zoezi hili shirikishi ni mwendelezo wa Mpango Maalum wa Usafishaji na Utunzaji wa Mazingira.

 
 
 
 

Pichani juu ni baadhi ya washiriki KIYOA na FADERATION wakati wa kuanza kwa muendelezo wa zoezi la usafi katika eneo la Tungi, Kigamboni, Dar es salaam. Mwenyekiti wa Serikali ya Mtaa wa Tungi, Ndg. Ramadhani Kayungi (mwenye fulana nyeusi) ni mmoja wa viongozi walioshiriki zoezi hilo.

 

Pichani chini zoezi likiendelea.

 
   

 



"Hapa mpaka kieleweke!!" Pichani chini ni Ndg. Godfrey Miunguzi (Mwenyekiti Msaidizi wa KIYOA) alisikika hapa akiwahamasisha washiriki.



  

Pichani chini, Washiriki kutoka KIYOA na FEDERATION waliojitoa kwa hali na mali wakikamilisha Awamu ya Pili ya muendelezo wa Mpango Maalum wa Usafishaji na Utunzaji wa Mazingira.

 



ILANI:

NI MARUFUKU KUTUPA TAKATAKA KATIKA MAENEO YOTE
AMBAYO ZOEZI HILI LIMEKWISHA FANYIKA. 
 
WATOA HUDUMA WA "KIYOA" NA "FEDERATION" WATAPITA MAJUMBANI NA KUZOA TAKA ZILIZIZALISHWA KWA UTARATIBU ULIOKWISHATOLEWA.
 
EPUKA MADHARA YA KUTOTII SHERIA, TII SHARIA BILA SHURUTI.
ZINGATIA USAFI WA MAZINGIRA KWA AFYA YAKO NA JAMII INAYOKUZUNGUKA

Friday, February 22, 2013

KIJANA AMKA! TUMIA KIPAJI ULICHONACHO


Neno "Kipaji" kwa Kiswahili chepesi ni uwezo mtu aliozaliwa nao ambao humwezesha kufanya jambo fulani vizuri. Mfano, kipaji kinaweza kuonekena pale mtu anapokuwa amefanya vizuri katika masomo, michezo kama vile mpira wa miguu, mpira wa kikapu, mpira wa mikono  na mambo mengine kama vile useremala; ushonaji; umeme, mapishi, uvuvi, uogeleaji, ulinzi, n.k. 

 

Jambo hili lililofanywa vizuri linaweza kuwa ni chanzo cha kupata umaarufu na mwishowe kumfanya mhusika kufahamika vyema katika jamii. Aidha, kuna faida nyingi ambazo mtu huzipata kutokana na kufahamika vyema katika jamii, faida hizo ni pamoja na kufahamiana na watu mbalimbali (networking) ambao ni moja ya chanzo kikuu cha mafanikio ya yeyote mwenye KIPAJI katika jamii.

 

KIYOA inapenda kukutia moyo ewe kijana kuwa, pamoja na changamoto nyingi zinazotukabili katika maisha yetu tunayoishi, ni vyema tukatumia vipaji tulivyonavyo ili viweze kutusaidia kutuunganisha na watu mbalimbali ambao wanaweza kuwa ni chanzo cha mafanikio katika kukabiliana na changamoto katika maisha yetu ya kila siku.

 

Kijana Amka!! Tumia Kipaji Ulichonacho!!!!

 
 
 
 

Pichani juu ni WanaKIYOA dada Itika Seme (mwenye koti) pamoja na dada Sara Richard wakipanga nguo mbalimbali walizozitengeneza ikiwa ni sehemu ya maonyesho ya Vipaji na kazi za mikono za WanaKIYOA. Maonyesho haya yalifanyika Chadibwa Beach, Kigamboni - Dar es Salaam.

 

Pichani chini ni baadhi ya watu waliofika kujionea maonyesho ya WanaKIYOA.

 
 
 
 

Baada ya kukamilika maonyesho na mauzo ya  kazi za mikono. Zoezi lililofuata ni kujumuika na jamii katika muziki. Pichani chini WanaKIYOA wakionyesha vipaji katika kucheza muziki 'KWAITO'.

 
 

 Pichani chini ni WanaKIYOA na Wanajamii wakionyesha VIPAJI katika muziki "MDUARA"

 


Thursday, February 21, 2013



ZOEZI LA USAFI WA MAZINGIRA LILILOFANYIKA TAREHE 16 FEBRUARI, 2013





 

Pichani juu ni baadhi ya vijana wa KIYOA wakianza utekelezaji wa ukusanyaji na uchomaji  takataka   zilizoonekana katika maeneo yanayozunguka nyumba za wakazi wa Tungi Kigamboni, Dar es Salaam. Lengo kuu la zoezi hili lilikuwa ni kuwakumbusha Wananchi juu ya umihimu wa ushiriki wa pamoja katika utunzaji wa mazingira yanayotuzunguka.





Pichani juu ni dada Joanitha Joas akiendelea na ukusanyaji wa takataka zilizosambaa katika makazi ya watu.

 

Pichani chini ni Wadada wa KIYOA wakiendelea na zoezi la ukusanyaji na uchomaji takataka.

 


Pichani  chini, zoezi la ukusanyaji na uchomaji takataka likiendelea katika eneo lililo katikati ya makazi ya watu na ambalo limekuwa likitumika kama dampo la takataka.




   Zoezi la ukusanyaji na uchomaji takataka hatua ya kwanza  lakamilika.  




UJUMBE KWA WANAJAMII


NI VYEMA SOTE KWA PAMOJA TUZINGATIE MAELEKEZO NA KANUNI ZA AFYA BORA KWA KUSHIRIKI  KATIKA UTUNZAJI MAZINGIRA YETU YANAYOTUZUNGUKA.

Aidha, kwa wakazi wa Tungi, Kigamboni Dar es Salaam. KIYOA inapenda kuwajulisha kuwa, utaratibu maalum wa ukusanyaji wa takataka umeandaliwa ambapo KIYOA wakishirikiana na FEDERATION watapita majumbani na kukusanya takataka zote zilizozalishwa kwenda kutupwa eneo lililoteuliwa. Wana-Tungi wote mnaombwa kutoa ushirikiano wakati wa zoezi hili. 

Monday, January 28, 2013


    "Umoja; Upendo na Mshikamano ndiyo nguvu yetu".

 

Pichani juu baadhi ya WanaKIYOA (kuanzia kulia) ni Ndg. Godfrey Miunguzi; Ndg. Shuma Mafuwe; Ndg. Greyson Mwikola; Ndg. Gerald Msuya; Ndg. Jimmy Mayunga muda mfupi kabla ya kuanza rasmi kwa Mkutano Mkuu wa KIYOA

 

Pichani chini ni baadhi ya WanaKIYOA na maeneo ya ushiriki wao katika KIYOA



    Dada Itika Seme - MwanaKIYOA (Uhamasishaji)




    Dada  Ghat Francis - MwanaKIYOA (Fedha na Utawala)




 Dada Victoria Zakayo - MwanaKIYOA ( Shughuli za Kijamii)



   Kaka Godfrey Miunguzi - MwanaKIYOA (Utawala; Maadili na Miradi)


MATUKIO KATIKA PICHA MKUTANO MKUU WA KIYOA ULIOFANYIKA BARAKUDA BEACH TAREHE 26 JANUARI 2013

KUMBUKUMBU ZA MUTANO MKUU WA KIYOA

Wajumbe wakipata chakula cha mchana kabla ya kuingia awamu ya pili ya kumalizia Mkutano Mkuu wa KIYOA.




 Pichani juu ni wajumbe wakimalizia  kupata chakula cha mchana.

 

UCHAGUZI WA UONGOZI MPYA WA KIYOA KWA MWAKA 2013

 

Pichani chini ni Ndg. Gerald Msuya (kushoto) ambaye alichaguliwa kuwa Mwenyekiti wa kusimamia   uchaguzi wa viongozi wapya wa KIYOA. Kulia kwake ni msaidizi wake dada Judy Isomba akimsaidia kuhesabu kura.

 

Katika uchaguzi huo Ndg. Humphrey Msulwa alichaguliwa kuwa Mwenyekiti; Ndg. Godfrey Minguzi amekuwa Mwenyekiti Msaidizi; Nafasi ya Katibu imechukuliwa na Ndg. Shuma Mafuwe; Ndg. Jimmy Mayunga amekuwa Katibu Msaidizi. Mwisho, nafasi ya Mhasibu (Mweka Hazina) imechukuliwa na Ndg. Ghati  Francis Changarawe.


     



MKUTANO MKUU WA KIYOA WA MWAKA 2012 WAMALIZIKA

Pichani juu ni baadhi ya WanaKIYOA wakitawanyika baada ya majadiliano ya zaidi ya masaa matano yaliyowawezeha kupata maazimio ya msingi katika utekelezaji wa kazi za KIYOA.


MATUKIO KATIKA PICHA YA MKUTANO MKUU WA KIYOA ULIOFANYIKA BARAKUDA BEACH TAREHE 26 JANUARI 2013



WANAKIYOA WAKISUBIRI KUANZA MKUTANO